Ndugu na dada yangu, Mungu anakuitaji jinzi ulivyo, hata kama wewe ni mkorofi, njoo kwa Yesu jinzi ulivyo, hata kama wewe ni kahaba, njoo kwa Yesu jinzi ulivyo.
Sisi zote tuliyo mpokea Kristo Yesu na kufanywa kuwa wana wa Mungu (Yohana 1:12), tulipewa nafasi katika ufalme wa Mungu na kuwa warithi pamoja na KRISTO YESU.
Imani ni kuwa na hakika ya mambo yatarajiwayo, bayana ya mambo yasiyo onekakana. Ni vyiema kuwa na imani, lakini ni muhimu pia kuifuatilia kwa matendo. kwa mfano ukiwa unatafuta kazi, unakuwa na imani ya kwamba utapata huo kazi, alafu unachukua hatua ya kwenda kuangalia huo kazi.
Ijapo Mungu anatupenda na upendo wanamna hii, tusisahau ya kwamba anachukia dhambi wala hauziki na dhambi. kwahivyo ukiruhusu dhambi ikutawale, dhambi itaweka mpaka kati yako na Mungu. Kwahivyo acha dhambi ili uishi maisha matakatifu.
Kuishi chini ya mamlaka ya ulimwengu inamanisha mambo unayo yafanya ni ya kiulimwengu yasiyo mpendeza Mungu. Kwa njia nyingine inamanisha, maisha yako yana fanana na ya wale ambayo hawaja mtambua Kristo.